Monday, December 17, 2012

Geuza Makosa Uliyopitia Mwaka 2012 Kuwa Darasa la Kuhitimu 2013

Wakati Watu Wakiwa Kwenye Pilika Pilika za Christmas na Zikiwa Zimebaki siku 13 kwa Msaada wa Mungu tumalize Mwaka 2012 na kuingia mwaka mpya wa 2013 kila mtu ana jambo la kuuongelea mwaka huu ambao unamalizika malizika. Ni Mengi yamepita mwaka 2012 na Mengine yakuchekesha na mengine ya kuliza lakini ndio mwaka unamalizika.


Tunapoelekea mwaka 2013 kuna baadhi ya Makampuni yamesha andaa viapaumbele vyao kwa ajili ya mwaka unaofuata, Kuna Familia kama Familia zimekaa na kupanga mipango yao kwa ajili ya Mwaka unaofuata na kuna watu binafsi ambao wao wamasha evaluate kwa mwaka 2012 na kuandaa mipango mbalimbali kwa ajili ya mwaka 2013.
Kwa utamaduni wetu wa Kitanzania tumejifunza kuwa kukosea ni kitu kibaya sana na tunatumia muda mwingi kujipanga tusikosee na inapotokea tumekosea hali tunayojisikia haitupi tena changamoto ya kujaribu tena jambo ila zaidi ya kuliogopa. Kama mtu aliwahi jaribu biashara mwaka 2012 halafu akapata hasara kinachotokea ni mtu huyo kuto kutaka kabisa kusikia kitu kinachoitwa Biashara kwenye maisha yake. Kama mtu aliingia kwenye mahusiano na mwisho wa siku kupitia mahusiano hayo akaumizwa basi kwenye ubongo wake na moyo wake anatokea kuchukia kitu kinachoitwa mahusiano. Kama alipata hasara kwenye Kilimo basi chochote unachomwambia kuhusu Kilimo kwake linageuka kuwa ni jambo la kulitazama mara mbili ama mara tatu sababu tayari ana kumbukumbu mbaya na Suala zima la Kilimo.
Kujitathimini na Kusahihisha kupitia makosa tunayoyafanya kwenye maisha ni jambo lenye kuleta maendeleo kwa kila mtu mwenye nia ya kuendelea mbele. Wahenga walisema tunajifunza kutokana na makosa. Kwenye Biblia ukisoma kuna story maarufu sana ya Mtu anaitwa "Mwana Mpotevu" yamkini hili iso jina lake halisia inawezekana anaitwa James, Anna, Rose ama hata Filikunjombe lakini kwa kumbukumbu njema akaitwa kwa sifa yake "Mwana Mpotevu" ukisoma vizuri huyu Kijana hakuwa amepotea alienda mahali kula bata wa kutosha baada ya kupata urithi. Yamkini Mwana Mpotevu hana tofauti sana na wengi wetu katika Maisha Chanzo cha fedha cha Mwana Mpotevu ni Urithi, yawezekana wewe Chanzo Cha Fedha ni Mshahara, ama Biashara matumizi ya kutapanya kama yale ya Mwana Mpotevu kila mtu anayo, Mwana Mpotevu angekuwa na Option ya kukopa kama wewe pengine angekopa, Mwana Mpotevu angekuwa na Option ya Mpesa angeomba kwa rafiki zake, tofauti ni kwamba wewe unaishi kwa madeni Mwana Mpotevu hakuwa na Option hata moja zaidi ya kula Chakula Cha Nguruwe. Tofauti inakuja kwenye Kuji Evaluate na Kuchukua hatua za mabadiliko Chanya. Wengi wetu tuna jitathimini lakini tunarudia makosa yale yale tunayoyafanya kila iitwapo leo. Hatua madhubuti za mabadiliko zimekuwa kwenye makaratasi na mioyoni lakini sio katika matendo.
Kubadilika kunahitaji discipline hasa unapoamua kubadilika kwa kuacha kitu unachokipenda, yamkini katika tathimini utabaini kuwa Usingizi na Kulala kusiko na sababu ndiko hasa kumesababisha uwe hivyo ulivyo sasa unapoamua kubadilika kuacha kulala kitu unachokipenda ni changamoto inayohitaji nidhamu. Yamkini utagundua asilimia kubwa ya matumizi ya fedha zako ni starehe, mavazi na anasa na umejikuta umekuwa haufanyi akiba ya fedha zako, usitegemee kabisa ukiamua kubadilika mambo yatakuwa rahisi kama unavyodhani inahitaji nidhamu.

Kuna makosa mengi sana yamkini tumefanya mwaka 2012 mengine kwa kutambua na mengine pasipo kutambua lakini mwisho wa siku matokeo yake hayakuwa ya kupendeza na kufurahisha, jitathimini kwa kina kwanini ulianguka, Usitazame tu wapi umeangukia bila kutazama kwanini ulianguka bila shaka itapekelekea wewe kuanguka tena na tena kwenye maisha. Kwanini usikae mahali ukajifungia ukatathimini mwaka 2012 ulikopita ukayatazama mazuri uliyoyafanya na kuongeza tija katika yale mazuri na ukayatathimini changamoto ulizokutana nazo mwaka 2012 na kuona ni namna gani ulichangamotika ili changamoto hizo uweze kuhitimu mwaka 2013. Ni Kujidanganya kuingia mwaka mpya bila kujua wapi unakwenda na nini unataka kufanya Kimaisha. Kurudia mambo yale yale na namna ile ile ya kufanya itasababisha tusipige hatua kwenye maisha yetu ya kila siku. Hatuwezi tukawa tunaishi kama wanyama wasio na akili wanaoishi kila siku bila kujua nini kinaendelea kwenye maisha yao. Kwa kadri miaka inavyokwenda ndivyo tunavyokaribia uzee na changamoto zake mwisho wa siku mambo miaka 10 ijayo tutajilaumu sana kwa mambo ambayo hatukuyafanya leo.
Bado unayo nafasi ya kujitathimini upya, jipange sawa sawa kukabiliana na changamoto za mwaka 2013 itakuwa ni ajabu jambo lile lile ulilochemsha mwaka 2012 ukachemsha mwaka 2013 kwa namna ile ile.

Think Differently and Make a Difference.

By
 
Papaa Ze Blogger.
0713 494110

iving Water Worship Team Wafanya Live Recording at Diamond Jubilee

Siku Moja Baada ya kundi Maarufu Africa Ya Kusini Joyous Celebration kufanya Live Recording yao ya Albam ya 17, Kundi Maarufu La Living Water Worship Team la Makuti Kawe Limefanya Live Recordings Katika Ukumbi Maarufu wa Diamond Jubilee.

Katika Live Recording hiyo iliyoingiza nyimbo takriban 17 ilihudhuriwa na Wakazi wengi wa Jiji la Dar-es-Salama na Vitongoji vyake. Shughuli nzima ya Event Hiyo iliongozwa na Ma Mc Papaa Ze Blogger Pamoja na Rose Mushi. Vikundi vilivyosindikiza Live Recording hiyo ni R.I.O.T Dancers, Glorious Celebration pamoja na John Lisu.
 Living Water Worship Team Wakiwa Back Stage kwa matayarisho
 Apostle Ndegi pamoja na Mke wake Lilian Ndegi wakienda Sawa.
                         Hudson Kamoga and Ze Blogger ndani ya Diamond
             Event Manager Ms. Delicious akienda sawa ndani ya Diamond. 
                                  Watu wakipokea kama kawa
                            Wengine wakakutana na Nguvu ya Mungu
 Kama ni Mpira basi tunasema ni Nyota ya Mchezo...Raphaaa ni Next Level Sana
                                Mzee Mzima John Lisu akiwa Kikazi Zaidi.
                                       Machine Ingine hii Rapha
                                          RIOT Dancers back stage
                        Phase Two ilikuwa amsha amsha sana siku ya Jana
                         John Lisu akiwa na Mkewa ndani Ya Diamond
                         Baba Askofu Prosper Mwakitalima akiwa Kazini
                         Glorious Celebration wakiwa Jukwaani
                         Living Water Jukwaani
                         Watu wakienda Sawa
                         Kama JC vile
                              Ma Mc wa Event Ya Jana Papaa Ze Blogger and Rose Mushi.